Sunday, February 22, 2009

WANAMUITA MR.BLUE




Ze king wa maposeeeeeeeeeee?

Wimbo uliomtoa ulikuwa ni ule uliokuwa ukiinadi rangi ya blue.Pengine ndicho chanzo cha yeye baadaye kuja kujulikana kama Mr.Blue.Pamoja na hayo wimbo wake ulioitwa “Mapozi” ndio ulikuja kutamba kwa staili ya aina yake.Baada ya hapo ikawa ni mapozi nawe,mapozi nawe.Lakini kwa mashabiki wa muziki wa kizazi kipya anabakia kuwa Mr.Blue.Hivi karibuni alikuwa katika ziara ya muziki nchini Uingereza.Ni miongoni mwa vijana walioko katika fani ya burudani kupitia muziki nchini Tanzania ambao wanaweza kusema “wanafanya vizuri” katika wanachokifanya.

No comments:

Post a Comment